10 December 2013

HIKI NDICHO WALICHOZUNGUMZA MASUPERSTAR WA BONGO KUHUSU SAKATA LA KUFANYA NGONO KINYUME NA MAUMBILE


Na Mwandishi Wetu
MADAI yameibuliwa kwamba asilimia 90 ya warembo mastaa wanajihusisha na mchezo mchafu wa mambo ya Pwani. 

Mastaa wawili, Baby Madaha ambaye ni mwanamuziki pia muigizaji na mtangazaji Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’ ndiyo waliolifichulia Uwazi wiki iliyopita.

Lulu alisema: “Mastaa wengi wakiambiwa watakataa lakini wana tabia mbaya, hivi sasa wanaona ndiyo fasheni.

“Hata wanaume kama mwanamke anakuwa mgumu kwenda kinyume, anamuona mshamba, tena wakati mwingine anakwambia mbona mwenzako anatoa.”

Lulu alipoulizwa kama yeye amewahi kujihusisha na mchezo huo alijibu: “Mimi sipendi kabisa, ila iliwahi kunitokea mara moja kipindi nilipokuwa na bwana wangu wa Kinzanzibari.

“Kwa kweli ni mateso makubwa. Kwanza yule mwanaume alinibaka, haikuwa ridhaa yangu na kunitenda hivyo nilimuacha. Nawaomba wengine waelewe kuwa ni jambo baya. Binafsi sitakuja kufanya katika maisha yangu yote.”

Lulu aliendelea kusema: “Mimi nina orodha ndefu ya mastaa wanaojihusisha na tabia hiyo, siwataji kwa sasa lakini zaidi ya asilimia 90. Unajua hivi sasa hata wanaume wanaotendwa mchezo mchafu ni wengi ndiyo maana wanawake wanaamua kuachia ili wasizidiwe kete na wanaume mashoga.”

Baby alisema: “Wanaojihusisha ni mastaa tena wenye majina makubwa na mamisi maarufu. Mara nyingi nawasikia wakizungumza hata wakilewa, wanaeleza kinagaubaga kuhusu michezo yao.

“Yaani ni noma, mbele ya fedha tena, watu wanakubali kwa tamaa zao. Mimi mwenyewe nilishaambiwa kuwa ni poa sana lakini moyo umekuwa mzito. Nashukuru sijawahi kuambiwa na mpenzi wangu yeyote kufanya hivyo.”

Mbali na hao, mastaa wengine waliozungumza na gazeti hili walikiri kukithiri kwa tabia hiyo na kutoa maoni yafuatayo;

MAIMARTHA JESSE
Anajulikana pia kama Oprah wa Bongo, alisema: “Wengi wanafanya hicho kitendo kwa tamaa na mihangaiko ya maisha. Kwangu mimi siwezi kufanya, kina athari kubwa kiafya na naomba watu wajue hilo.”

JULIET WILLIAM
Mshindi wa taji la dunia la Miss Progress International, pia Miss Tanzania namba tatu mwaka 2009, alisema: “Mtu anayefanya kitendo hicho kwangu hana thamani, hicho kitendo siyo kizuri kwani kinakwenda kinyume na matakwa ya Mwenyezi Mungu.”

UMMY WENSLAUS ‘DOKII’
Staa huyo wa filamu alisema: “Watu wanaofanya kitendo hicho bila shaka watakuwa na matatizo ya akili. Wanatembea chini ya laana.”

MAUNDA ZORRO
Mwanamuziki huyo alisema: “Mtu anayefanya mapenzi kinyume na maumbile hajui maadili ya Mwafrika. Mwanaume anayemtamkia mwanamke kuhusu kitendo hicho ujue hana malengo naye, anataka tu kumchezea.”


JACQUELINE PENTZEL 
Alisema: “Aku, mimi sijawahi kufanya hayo mambo, ni dhambi mbele ya Mungu na wanaofanya pengine akili zao ni pungufu.”

COLETHA RAYMOND
“Sipendi kitendo hicho, kama ningekua na mume anayependa kufanya mchezo mchafu  ningemwacha haraka sana.”

STARA THOMAS
“Wanaofanya tendo la ndoa kinyume na maumbile hawajui thamani ya utu wao, kitendo hicho ni cha kijinga na ni ushamba. Wahusika wakuu wanatakiwa kufikiri vizuri juu ya jambo hili kwani hushusha thamani ya utu.”

-GPL

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname