Makocha David Moyes na Louis van Gaal wameendelea kufananishwa kwa utendaji wao katika benchi la ufundi la Old Trafford.
Mwanzoni
mwa msimu wakati mholanzi Louis van Gaal alipokuwa na matokeo mabaya –
vyombo vya habari vilikuwa vikitoa takwimu mara kwa mara na kumfananisha
na kocha aliyefukuzwa Man United – David Moyes. Safari hii zimetolewa
takwimu za makocha hao katika kuiongoza Man United katika mechi dhidi ya
timu kubwa sita za juu.
LVG
amemuacha mbali Moyes – akiwa na ameshinda asilimia 62.5% ya mechi dhidi
ya vilabu vya Top 6 huku David Moyes akiwa na rekodi mbaya ya kushinda
8.33% tu ya mechi hizo.
Manchester
United walipata taabu mwanzoni mwa msimu lakini hivi karibuni wamekuwa
kwenye kiwango kizuri wakizifunga timu Tottenham, Liverpool, Aston Villa
na jana wakaipa kipigo cha mbwa mwizi Man City.
David
Moyes aliweza kushinda mechi moja tu kati ya 12 alizoiongoza United
dhidi ya Vilabu 6 bora kwenye ligi na United wakamaliza ligi wakiwa
nafasi ya 7.
United
sasa wanashika nafasi ya 3, wakiwa wanaongoza kwa kupata matokeo mazuri
dhidi ya timu zote za Top 6 – huku wakiwa wamebakiwa na mechi 2 tu za
vilabu vya juu – Chelsea na Arsenal – lakini Van Gaal ameshaiongoza
United kushinda mechi 5 kati ya 8 alizocheza.
LOUIS VAN GAAL VS DAVID MOYES
No comments:
Post a Comment