04 February 2016

NAY WA MITEGO ATOA KAULI KUHUSU MWIGIZAJI RAY KAWA MKONGO MPAKA LEO ANAISHI KWAO

Msanii wa muziki wa bongo fleva Nay wa mitego ameweka wazi baadhi ya mistari ambayo ipo kwenye moja ya wimbo wake ambao ana wasiwasi kuuachia kwa mashabiki kutokana na vitu alivyozungumza.
Kwenye wimbo huo ambao anadai anaogopa akiuachia watanzania watamchukia kwa mambo aliyozungumza kwenye wimbo huo alioupa jina la ‘Shika adabu yako’.


Katika wimbo huo Nay wa Mitego ametaja majina ya watu maarufu na kuwapa maneno yake kutokana na kile ambacho yeye anakifahamu na kukiamini.
Moja ya jambo alilozungumzia kwenye wimbo huo ni kuhusu tasnia ya movie na kusema imekufa wamebaki kuuza sura na wote wanataka kuimba kama Shilole na Snura.
Pia ameonekana kumchana Ray kwa kusema kuwa mpaka sasa anaishi kwao na pesa anazopata kuuza movie ananunua mkorogo.


“Mungu hakunyimi vyote lazima atakupa chako, demu ana sura mbaya lakini na bonge la tako. Bongo Movie imekufa wamebaki kuuza sura, wote wanataka Kuimba Kama Shilole Snura. Ray Kigo kawa Mkongo mpaka leo anaishi kwao, hela za kuuza Movie zote ananunua mkorogo, haitoki hii nimeirecord tu yakusiliza na wanangu maskani maana mtanichukia kwa niliyozungumza humu” Alisema Nay wa Mitego.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname