Mh Mbowe
Katika hali isiyokuwa ya
kawaida, mwenyekiti wa CHADEMA, mhe Mbowe, amemuangukia Zitto na
kueleza namna ambavyo yeye na chama chake wamemkosea Zitto wakati huo
Zitto akiwa mwanachama na kiongozi wa CHADEMA.
Mbowe ameyasema hayo katika mahojiano na gazeti la Mwananchi na kueleza yafuatayo:
“Hatujawahi kama kambi
ya upinzani kumtenga Zitto kwenye kila jambo, yapo mambo tunaweza
kulazimika kutengeneza ushirikiano na wabunge hata wa CCM ili kufanya
jambo fulani kutekelezeka.
“Kushirikiana na Zitto
si jambo la ajabu kama ambavyo umeona tukilifanya. Yapo majeraha mengi
ambayo tumeyapitia pande zote (CHADEMA na Zitto) ambayo huwezi kuyatibu
kwa siku moja. Yapo ambayo yatapona kulingana na muda. Unaweza kumfanyia
mtu kitu kibaya, lakini baadaye ukatambua kuwa umekosea. Chochote
katika siasa kinawezekana,” alisema Mbowe.
Zitto alifukuzwa Chadema
na kujiunga na ACT Wazalendo Machi 21, 2015 chama ambacho hakina
ushirikiano na vyama vinavyounda Ukawa lakini katika siku za karibuni
ameonekana kuwa karibu na umoja huo wa wananchi, ikiwa ni pamoja na
kushirikiana kuibua hoja mbalimbali katika mkutano wa Bunge unaoendelea
mjini Dodoma.
Source: Mwananchi
No comments:
Post a Comment