24 October 2014

MAKAVU LIVE: DIAMOND PLATINUMZ, KUNA KITU CHA KUJIFUNZA!


NASIB Abdul, ambaye uwezo wake wa muziki wa kizazi kipya umempatia jina la Diamond Platnumz, mwishoni mwa wiki iliyopita katika tamasha la Fiesta, paleLeaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, itabaki kuwa ndani ya kumbukumbu zake, angalau kwa miaka kadhaa ijayo.

Mamia ya mashabiki waliojazana katika viwanja hivyo, walimzomea kwa nguvu kubwa, tofauti na matarajio ya wengi kwamba angefunika, kama wenyewe wanavyosema. Kelele zile za kuzomewa zilimshtua hadi Diamond mwenyewe, ambaye alikiri jukwaani pale kwamba haikuwa bure, lazima kulikuwa na kitu. 




Baada ya tukio lile, watu wameongea mengi sana, ikiwa ni pamoja na propaganda kwamba zomeazomea ile ilipangwa. Na nani? Hapo ndipo penye kizungumkuti. Wengine wanasema eti mashabiki wa Ali Kiba ndiyo walipanga ili kumuonyesha kwamba yeye hakuwa bora zaidi ya msanii wao. 
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI>>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname