30 December 2015

MASTAA DAVIDO NA TEKNO WANACHNGIA PENZI LA AGNES MASOGANGE

Aggy31Agnes Masogange.
RIPOTI zimesambaa kwamba wanamuziki nyota wawili wa Nigeria, Davido na Tekno, huenda wanachangia penzi la mrembo wa Kitanzania, Agnes Masogange.

Mwezi Novemba mwaka huu mwimbaji Davido ambaye alivuma na album ya Omo Baba Olowo (Mtoto wa Tajiri) alijirusha na wasichana kadhaa wakati wa bethidei yake na mmoja wao alikuwa Masogane na baadaye zikaenea habari kwamba alikuwa mjamzito akitegemewa kumzalia Davido mtoto wa pili, lakini habari hizo baadaye zikakanushwa.
image (5)…..Akiwa na Tecno.
Kitu cha ajabu ni kwamba Masogange alianza kuweka na kufuta ujumbe mbalimbali kwenye mtandao ukionyesha alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Tekno kwa kula naye bata katika hoteli moja nchini Afrika Kusini.
Agnes-na-Davido
Tekno naye alianza kutuma ujumbe kama huo, jambo lililowafanya mashabiki wake kuamini alikuwa na uhusiano na msichana huyo. Hata hivyo, mwimbaji huyo ameufuta ujumbe wote huo katika ukurasa wake.
CHANZO;GPL

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname