Aliyekuwa
mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa jana hakuhudhuria
mkutano wa kampeni za ubunge mjini Arusha kwa maelezo kuwa anajiandaa
kutoa tamko kuhusu hali ya kisiasa visiwani Zanzibar.
Maelfu
ya wafuasi wa Chadema jana walifurika kwenye Uwanja wa Ngarenaro mjini
hapa kuhudhuria kampeni za ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini ambao
uliahirishwa kutokana na kifo cha mgombea kutoka chama cha ACT
Wazalendo, lakini wakakumbana na tangazo kuwa Lowassa hataweza kuhutubia
na badala yake atakuja siku ya kufunga kampeni hizo..
No comments:
Post a Comment