Serikali imeahidi kumchukulia Shilole kufuatia kusambaa kwa picha zake chafu zilizopigwa wakati akitumbuiza nchini Ubelgiji.
Akizungumza bungeni Dodoma
leo, Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Juma Mkamia,
wakati akijibu hoja za wabunge baada ya kusoma makadirio na matumizi wa
wizara hiyo, alisema tayari serikali imeliagiza baraza la sanaa taifa
BASATA kufanya naye mahojiano.
Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Juma Mkamia
“Tumemtaka ajieleze kupitia
BASATA, akishajieleza serikali itachukua hatua na niombe mheshimiwa
spika kupitia bunge lako tufuku, kuliomba radhi kwa upande wa serikali
kwa kitendo kilichofanywa na mwanamuziki yule. Sio maadili yetu na
nimesema akishajieleza serikali itachukua hatua yake,” alisema Juma
Mkamia
No comments:
Post a Comment