Kama umedownload au kutumiwa wimbo unaosemekana kuwa ni wa Diamond
featuring P-Square na pamoja na kuusikiliza kwa mara kibao ukashindwa
kusikia sauti ya Paul au Peter Okoye, basi sikio lako halikudanganyi –
hakuna collabo hiyo.
Wimbo huo unaitwa ‘Marry Me’ ni wa Iyanya ambao kipindi muimbaji huyo wa
Nigeria amekuja kwenye Fiesta mwaka juzi, alimpa nafasi Diamond
kuingiza kitu kwakuwa alisafiri na producer wake, Tekno aliyetembea na
vifaa vya muhimu vya studio. Kwenye wimbo huo Diamond hakuimba serious
na infact aliimba freestyle tu, kwa mujibu wa maelezo ambayo meneja wa
Diamond ameyatoa kwa Bongo5.
Wimbo original upo kwenye album ya Iyanya iitwayo ‘Desire’ (Iyanya vs. Desire)
iliyotoka February 6, 2013. Kwahiyo Iyanya alitaka kutengeneza remix ya
wimbo huo ambayo hata hivyo haikuweza kujumuishwa kwenye album hiyo.
Blog kadhaa za Bongo zimeupost wimbo huo kama wimbo wa Diamond
aliowashirikisha P-Square kitu ambacho si kweli. Hakuna shaka kuwa hiyo
ni collabo inayosubiriwa kwa hamu sana.
Marry Me ni ngoma kali hata hivyo, isikilize hapo chini.
No comments:
Post a Comment