Madaktari
nchini India wametoa meno 232 kutoka katika mdomo wa kijana mwenye umri
wa miaka 17, katika upasuaji uliochukua saa saba.
Kijana huyo Ashik Gavai alifikishwa hospitali akiwa amevimba na maumivu kwenye taya na shavu lake la upande wa kulia, amesema Dokta Sunada Dhiware, mkuu wa idara ya meno katika hospitali ya JJ jijini Mumbai.
Kijana
huyo amekuwa akisumbuliwa kwa miezi 18, na alilazimika kusafiri kwenda
mjini, baada ya madaktari katika kijiji chake kushindwa kufahamu chanzo
cha tatizo.
No comments:
Post a Comment