Toka March 8 2014 mpaka leo ikiwa ni
May, ndege ya Malaysia iliyokua imebeba zaidi ya watu 200 haijulikani
ilipo baada ya kupotea ikiwa inatokea Malaysia kwenda Beijing China.
Kwa siku zote hizo toka imepotea
ndugu wa abiria wa ndege hiyo wamekua wakishinda kwenye hoteli ambazo
pia zimekua zikitumiwa na shirika hilo la Malaysia kukusanyika na kutoa
taarifa kuhusu kinachoendelea kwenye kuitafuta ndege hiyo.
May 1 2014 taarifa zimeanza kusambaa
kwamba ndugu hao sasa wamepewa maagizo waondoke kutoka kwenye hoteli
zote walizofikia Beijing na Kuala Lumpar na kurudi nyumbani kwao ambapo
taarifa za chochote kitakachotokea watazipata wakiwa hukohuko majumbani.
Hii iliwafanya ndugu kadhaa kuangua tena vilio na kupiga mayowe baada
ya kujua kwamba taarifa ya shirika hilo la ndege inamaanisha
haitakuwepo tena ile mikusanyiko ya kila siku kwenye chumba cha mikutano
kwa ndugu hao kupewa taarifa za kinachoendelea kwenye zoezi la
utafutaji wa ndege hiyo.
Kwenye hoteli ya Lido Beijing ambako
kampuni hiyo ya ndege imekua ikiwalipia ndugu hao wa abiria toka ndege
ipotee, kulikua na watu wanaozidi 500 ambao wote ni ndugu wa abiria
waliopotea.
Hata hivyo kampuni hii ya ndege
itaanza kutoa malipo ya pesa kwa ndugu hao siku za karibuni ambapo japo
haijasema itatoa kiasi gani, sheria inasema ndugu wanaweza kulipwa
kuanzia dola za kimarekani laki moja na nusu mpaka laki moja na elfu 75.
Ripoti mpya iliyotoka inasema maafisa
hawakua wamegundua kupotea kwa ndege hiyo mpaka dakika 17 baadae na
walichelewa kwa dakika 240 kuanza kuitafuta ndege hiyo baada ya kupotea
kwenye radar.
No comments:
Post a Comment