MTU
mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Shija Machiya (30), mkazi wa Kijiji
cha Butulwa, Kata ya Old Shinyanga alizua kizaazaa, baada ya kupanda
kwenye nguzo ya umeme ya njia kuu inayopeleka umeme mgodi wa dhahabu wa
Bulyanhulu wilayani Kahama.Machiya
alipanda katika nguzo hiyo inayosafirisha umeme wa msongo wa KV 220
katika eneo la Ihapa jirani na Kiwanda cha Nyama na kusababisha taharuki
kwa wakazi wa maeneo hayo.Tukio
hilo lilitokea saa5 asubuhi, ambapo wakazi wa eneo hilo waliacha
shughuli zao kwa muda wakifuatilia tukio hilo pamoja na kuhofia maisha
mtu huyo.Mama mzazi wa Machiya, Mondesta Madirisha, alisema kuwa kwa
kipindi cha wiki moja mtoto wake huyo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kuchanganyikiwa akili.Alisema
kuwa wanahisi kuwa tatizo hilo lilitokana na kuugua malaria ambapo
waliamua kumpatia dawa za kienyeji na hali yake ilionyesha kuwa ni ya
kuridhisha.“Tulipompa
dawa ya kienyeji alipona kabisa, lakini jana tu kwenye mida ya saa
mbili asubuhi, hali yake ilibadilika ghafla. Alianza kupiga kelele,
akatoroka nyumbani na kuanza kukimbia ovyo barabarani, hali ambayo
ilisababisha baadhi ya wananchi kuanza kumfuata,”alisema Madirisha na
kuongeza:Bofya hapa inaendelea >>>>>>
No comments:
Post a Comment