Mwanafunzi
wa Eden Hilling College aliyetajwa kwa jina la Atu Gabriel amefariki
akidaiwa kujaribu kutoa mimba kwa kunywa vidonge.Kwa mujibu wa Kamanda
wa Polisi mkoa wa Pwani (RPC), Orech Mtei, katika kuthibitisha kutokea
kwa tukio hilo, alisema Jumamosi April 26 mwili wa Atu ulikutwa katika
chumba cha mwanaume aliyefahamika kwa jina la Hafidhi ambaye anadaiwa
kuwa mpenzi wake.Kamanda Mtei ameeleza kuwa polisi walikuta mwili wa
marehemu ukiwa karibu na vidonge alivyotumia huku akitokwa damu nyingi
sehemu za siri na kwamba polisi wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa Hafidhi
ambaye alidaiwa kukimbia baada ya tukio."Ni kweli tukio hilo limetokea
Jumamosi Aprili 26 mwaka huu eneo la Kwa Mfipa baada ya jeshi letu
kutaarifiwa kuwepo kwa mwili huo na polisi walipofika na kufanya
uchunguzi wake tulibaini marehemu alifariki dunia kaika jaribia la
utoaji wa mimba.....hata hivyo mwili bado upo Hospitalini Tumbi kwa ajili ya uchunguzi zaidi," alisema Kamanda Mtei.
Kamanda
Mtei alisema mara baada ya kutokea kwa tukio hilo, kijana aliyetajwa
kwa jina la hafidhi ambaye inadaiwa alikuwa mpenzi wake alitokewa eneo
la tukio na jeshi hilo kwa sasa linamtafuta kwa ajili ya mahojiano zaidi
kabla ya kufikishwa mahakamani.

"Baada
ya tukio mtuhumiwa alikimbia na hadi sasa bado haijulikana alipo, jeshi
letu linaendelea kumtafuta popote alipo na mara baada ya kumpata
tutamuhoji na baadae atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua za
kisheri," alisema Mtei.
INAENDELEA HAPA
INAENDELEA HAPA
No comments:
Post a Comment