28 April 2014

Mwanafunzi wa chuo afia chumbani wakati akijaribu kutoa mimba

Mwanafunzi wa Eden Hilling College aliyetajwa kwa jina la Atu Gabriel amefariki akidaiwa kujaribu kutoa mimba kwa kunywa vidonge.Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani (RPC), Orech Mtei, katika kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo, alisema Jumamosi April 26 mwili wa Atu ulikutwa katika chumba cha mwanaume aliyefahamika kwa jina la Hafidhi ambaye anadaiwa kuwa mpenzi wake.Kamanda Mtei ameeleza kuwa polisi walikuta mwili wa marehemu ukiwa karibu na vidonge alivyotumia huku akitokwa damu nyingi sehemu za siri na kwamba polisi wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa Hafidhi ambaye alidaiwa kukimbia baada ya tukio."Ni kweli tukio hilo limetokea Jumamosi Aprili 26 mwaka huu eneo la Kwa Mfipa baada ya jeshi letu kutaarifiwa kuwepo kwa mwili huo na polisi walipofika na kufanya uchunguzi wake tulibaini marehemu alifariki dunia kaika jaribia la utoaji wa mimba....
.hata hivyo mwili bado upo Hospitalini Tumbi kwa ajili ya uchunguzi zaidi," alisema Kamanda Mtei.
Kamanda Mtei alisema mara baada ya kutokea kwa tukio hilo, kijana aliyetajwa kwa jina la hafidhi ambaye inadaiwa alikuwa mpenzi wake alitokewa eneo la tukio na jeshi hilo kwa sasa linamtafuta kwa ajili ya mahojiano zaidi kabla ya kufikishwa mahakamani.

"Baada ya tukio mtuhumiwa alikimbia na hadi sasa bado haijulikana alipo, jeshi letu linaendelea kumtafuta popote alipo na mara baada ya kumpata tutamuhoji na baadae atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua za kisheri," alisema Mtei.
INAENDELEA HAPA

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname