16 July 2014

FAHAMU DAWA YA KUTUNISHA MISULI

Pengine  ni katika harakati za kuutafuta utanashati  au  ukosefu wa ajira,  na huenda ikawa ni mtindo wa kimaisha kwa vijana wengi hapa nchini na duniani kote wanaotunisha misuli. Hata hivyo wanaume walio katika harakati za kutunisha misuli au kupata maumbo yenye miraba minne, wamekuwa wakitumia dawa ili kuyapata maumbo hayo badala ya kufanya mazoezi  ya viungo.

Vijana wengi hivi sasa  wananunua kwa wingi dawa za kutunisha misuli maarufu kama ‘doping’ kwa sababu zinazotajwa kuwa ni kutafuta ajira kama vile ulinzi kwenye kumbi za starehe, ulinzi wa watu maarufu(bodyguard) na wengine mashindano ya kunyanyua vitu vizito huku wengine wakiutafuta utanashati.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname