
STAA wa muziki wa bongo fleva nchini, Abdul Nassib "Diamond" ametakiwa kutokanyaga kabisa nchini China na kwamba akitokeza pua yake nchini humo asahau kabisa kurudi uraiani...
Hiyo inafuatia kijana mmoja mtanzania kukamatwa wiki iliyopita uwanja wa ndege wa Macau China na kudai kuwa yeye ni mcheza shoo wa mwanamuziki Diamond kutoka Tanzania....
Habari kutoka Macau China zinadai kuwa kijana huyo aliyejulikana kwa jina moja la Manyota alikamatwa akiwa kwenye harakati za kuingiza mzigo huo wa dawa za kulevya kwa kupitia uwanja wa ndege wa Macau....
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, inaarifiwa kuwa Manyota alikamatwa Alhamisi ya wiki iliyopita katika uwanja uleule aliokamatwa mtanzania mwingine Jackline Patrick, anayesotea rumande mpaka hii leo huko huko Macau China.
No comments:
Post a Comment