Stori: Shakoor Jongo
ILI kulinda heshima ya ukurugenzi, Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Choki amevuta mkoko Toyota Prado yenye thamani ya shilingi milioni 52.
ILI kulinda heshima ya ukurugenzi, Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Choki amevuta mkoko Toyota Prado yenye thamani ya shilingi milioni 52.
Mkoko mpya wa Ally Choki aina ya Toyota Prado ofisi za GPL.
Choki amenaswa na ndinga hiyo juzikati jijini Dar ambapo paparazi wetu
alipomuuliza sababu za kuongeza ndinga hiyo ilihali ana magari mengine
likiwemo Toyota Noah, Choki alitaja kigezo cha heshima kuwa sababu
iliyomfanya anunune ndinga hiyo.
“Unajua kila kitu kinakwenda na mipango lakini wakati mwingine heshima
ya mtu inajengwa na vitu vidogovidogo hivyo niliona angalau ndinga kama
hii inaendana na mimi, siyo kwamba nimenunua kuonesha jeuri, hapana
lakini heshima nayo inahusika barabarani,” alisema Choki.
Kuhusu suala la kujipendelea kununua magari yeye kama mkurugenzi, Choki
alisema yeye na bendi yake huwa hawana matatizo ya magari ya kusafiria
ndiyo maana wana magari zaidi ya saba yanayotumika kwa shughuli za
bendi.
Choki kama mkurugenzi na muimbaji, anakuwa mwanamuziki wa kwanza kumiliki gari la thamani katika wanamuziki wa dansi Bongo
Choki kama mkurugenzi na muimbaji, anakuwa mwanamuziki wa kwanza kumiliki gari la thamani katika wanamuziki wa dansi Bongo
No comments:
Post a Comment