Nyota wa muziki kutoka Uganda, Eddy Kenzo anatajwa kununua gari aina
ya Mercedes Benz kwa zaidi ya shilingi M100 za Uganda, ikiwa ni pesa
nyingi kabisa kuwahi kutumia kufanya manunuzi.
Ununuzi wa gari hilo, unaongeza idadi ya magari ambayo tayari
anamiliki msanii huyo, ikiwepo Prado TX, Regius na BMW X5, ikiwa ni
ishara ya akaunti za msanii huyo kuendelea kutuna kutokana na mafanikio
yake kimuziki.
Mwanamuziki huyu ameweka katika mtandao picha ya gari hilo jipya kama
njia ya kuhamasisha mashabiki wake kuwa inawezekana kufanikiwa pale
wanapokuwa wamejituma kufanya kazi.
“V8 compressor AMG, 320 for Bosses #mussuuza”
No comments:
Post a Comment