05 February 2016

Hii ndio Mercedes Benz ya Eddy Kenzo,ni milioni 100 za Uganda.

eddy
Nyota wa muziki kutoka Uganda, Eddy Kenzo anatajwa kununua gari aina ya Mercedes Benz kwa zaidi ya shilingi M100 za Uganda, ikiwa ni pesa nyingi kabisa kuwahi kutumia kufanya manunuzi.
Ununuzi wa gari hilo, unaongeza idadi ya magari ambayo tayari anamiliki msanii huyo, ikiwepo Prado TX, Regius na BMW X5, ikiwa ni ishara ya akaunti za msanii huyo kuendelea kutuna kutokana na mafanikio yake kimuziki.
Mwanamuziki huyu ameweka katika mtandao picha ya gari hilo jipya kama njia ya kuhamasisha mashabiki wake kuwa inawezekana kufanikiwa pale wanapokuwa wamejituma kufanya kazi.
 kenzo 1
V8 compressor AMG, 320 for Bosses #mussuuza

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname