23 June 2015

Wema:Jamani Nikiwa Bungeni Sitaongea Hivyo

 http://www.bongomovies.com/public/uploads/Wema_sepetu211.JPG
Staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu ambaye ametangaza nia ya kugombea nafasi ya ubunge wa viti maalumu Singida,amesema anafurahishwa na kitendo cha mashabiki wake kumwigiza sauti akiwa bungeni kwa  kuwa wameonyesha kumkubali kabla hajafika ‘Mjengoni’.
Alisema sauti hiyo inayomuigiza alitumiwa kupitia simu yake na haikumkwaza zaidi ya kufurahia  kwamba watu wengi wanakubali awe bungeni.
“Nafurahi kwa kuwa wengi wameshanipeleka bungeni wakati mimi ndiyo kwanza nipo katika harakati  za kuomba kuchaguliwa kupitia umoja wa wanawake Singida , lakini nafurahia kwa kuwa inaonyesha wengi wananikubali,  ila nikipitishwa kuwawakilisha wana Singida bungeni sitaongea kama walivyonirekodi katika sauti hiyo,” alisema Wema kwa furaha.
Mtanzania

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname