24 June 2015

ALI KIBA ATIMULIWA KWENYE NYUMBA! JOKATE ADAIWA KUWA CHANZO!


Nyota wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba. Waandishi Wetu
LICHA ya mwenyewe kukanusha vikali lakini madai mazito yanasema kuwa, nyota wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ametimuliwa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi iliyopo Kunduchi-Beach jijini Dar baada ya kukosana na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake ambaye pia ndiye mmiliki wa mjengo huo. 
Habari kutoka kwa chanzo makini zinaeleza kuwa, pamoja na Kiba kuendelea kusisitiza kwamba si kweli, mwanamke huyo anayeishi nchini Singapore, aliamua kuchukua uamuzi huo baada ya kusoma kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari kuwa, kwa sasa Kiba anatoka na Miss Tanzania namba 2, 2006, Jokate Mwegelo ëKidotií huku Kiba mwenyewe akikataa madai hayo. 

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname