10 November 2014

NUH MZIWANDA AJITETEA KUHUSU KUPEWA KICHAPO NA SHILOLE

MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva , Nuh
Mziwanda amefunguka kuwa watu
wanaomsema vibaya kuhusu yeye kupewa
kichapo na mpenzi wake , Zuwena Mohamed
‘ Shilole’ wanakosea kwani anaamini kufanywa

hivyo ni mahaba .
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi
karibuni, Mziwanda alisema kuna taarifa
zimeenea kuwa huwa anapigwa na Shilole
pindi anapokosea lakini ukweli si kupigwa
‘ live’ bali ni kupigwa kimahaba .
“ Jamani kupigwa wanakozungumzia watu
sielewi lakini mimi ananipiga kimahaba ,
wanaosema kuwa mpenzi wangu ananipiga
washindwe, watuache kwa raha zetu , ” alisema
Shilole.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname