BAADA ya kuachana na mkewe ambaye ni mtangazaji wa kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kinachorushwa na Redio Times, Hadija Shaibu ‘ Dida, ’ mtangazaji wa kituo cha Televisheni cha TV1, Ezden Jumanne ametaja sifa za mwanamke atakayekuja kumuoa kama akitaka kufanya hivyo.
Mtangazaji wa kituo cha Televisheni cha TV1 , Ezden Jumanne . Akizungumza na mwandishi wetu nyumbani kwake, Kijitonyama jijini Dar , Ezden alisema kuwa kutokana na kupitia kipindi kigumu cha kuachana na aliyekuwa mkewe amedai kuwa hafikirii kuoa kwa sasa lakini kama akija kuoa tena atamhitaji
mwanamke mcha - Mungu , mwenye heshima, asiye mlevi na atakayejitambua kama ni mke wa mtu.
“Sidhani kama nitaoa hivi karibuni , lakini kama nitaoa tena mwanamke ninayemtaka ningependa awe mwenye heshima, anayefuata dini, asiyependa ulevi na atakayejitambua kama mke wa mtu, ” alisema Ezden .
24 July 2014
MUME WA ZAMANI WA SUPER STAR DIDA SASA AANZA SAFARI MPYA YA KUSAKA MUKE SOMA HAPA LIVE!!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment