26 November 2013

TUNAOMBA RADHI KWA HIZI PICHA....17 WAJERUGIWA KATIKA AJALI YA HIACE HUKO KAHAMA..............CHEKI HAPA!!


Askari polisi akiwa akichukua maelezo kwa majeruhi kwenye wodi ya wanau



Watu 17 wamejeruhiwa baada ya gari la abiria walilokuwa wakisafiria kutoka ulowa kwenda mjini kahama kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Nyandekwa wilaya ya kahama mkoani Shinyanga.


Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ikilihusisha gari namba T 208 AGE lilokuwa likiendeshwa na dereva aliyetajwa kwa jina la Rashid Ramadhan mkazi wa Kahama mjini, ambaye hata hivyo alitoroka baada ya tukio hilo.

Kwa mujibu wa daktari mfawidhi wa hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga, jumla ya majeruhi 5 wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa huku 12 wakiwa wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.



Mganga mfawidhi wa hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga akiongea na waandishi wa habari

Daktari Nyaga amewataja waliolazwa kuwa ni Elizabert Mgesa (49), Katarina Makoye (32), Eliza Timotheo (30), Ngeke Chanila (23), Zawadi Andrea (18), Amos Hussein (32) na Adam John (20) ambaye alikuwa kondakta wa gari hilo.

Wengine ni Zakaria Leonce (25), Mabala Paulo (28), Hamis Makala (26), John Marcel (26) na Michael Rashid (47) na motto benad Paulo mwenye umri wa miezi mitano na kwamba wote hali zao zinaendelea vizuri.

Jeshi la Polisi wilayani kahama limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba uchunguzi wakubaini chanzo chake unafanywa, huku juhudi za kumtafuta dereva wa gari hilo zikiendelea.



Majeruhi akiwa na ndugu yake ambaye amekwenda kumtembelea
Mwandishi wa habari na mtangazaji wa redio kahama fm akichukua maelezo kwa mama Eliza aliyejeruhiwa
Askari wa usalama barabarani akichukua amelezo kwa majeruhi kwenye wodi ya wanawake
Ajabu sana: Majeruhi wawili wakiwa katika kitanda kimoja
Mama aliyejeruhiwa pia katika ajali hiyo
Mgonjwa akiwa amepumzika baada ya kupatiwa huduma
Miongoni mwa waliopata ajali akiwa kitandani wodini
Dada huyu akiwa ametulia kitandani kumuomba mungu ampe ahueni
Majeruhi wawili katika kitanda kimoja kama inanvyoonekana

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname