Watu 17 wamejeruhiwa baada ya gari la
abiria walilokuwa wakisafiria kutoka ulowa kwenda mjini kahama kuacha
njia na kupinduka katika kijiji cha Nyandekwa wilaya ya kahama mkoani
Shinyanga.
Ajali hiyo imetokea leo asubuhi
ikilihusisha gari namba T 208 AGE lilokuwa likiendeshwa na dereva
aliyetajwa kwa jina la Rashid Ramadhan mkazi wa Kahama mjini, ambaye
hata hivyo alitoroka baada ya tukio hilo.
Kwa mujibu wa daktari mfawidhi wa
hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga, jumla ya majeruhi 5
wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa huku 12 wakiwa wanaendelea na matibabu
hospitalini hapo.
Mganga mfawidhi wa hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga akiongea na waandishi wa habari
Daktari Nyaga amewataja waliolazwa kuwa
ni Elizabert Mgesa (49), Katarina Makoye (32), Eliza Timotheo (30),
Ngeke Chanila (23), Zawadi Andrea (18), Amos Hussein (32) na Adam John
(20) ambaye alikuwa kondakta wa gari hilo.
Wengine ni Zakaria Leonce (25), Mabala
Paulo (28), Hamis Makala (26), John Marcel (26) na Michael Rashid (47)
na motto benad Paulo mwenye umri wa miezi mitano na kwamba wote hali zao
zinaendelea vizuri.
Jeshi la Polisi wilayani kahama
limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba uchunguzi wakubaini
chanzo chake unafanywa, huku juhudi za kumtafuta dereva wa gari hilo
zikiendelea.
Majeruhi akiwa na ndugu yake ambaye amekwenda kumtembelea
Ajabu sana: Majeruhi wawili wakiwa katika kitanda kimoja
Mama aliyejeruhiwa pia katika ajali hiyo
Mgonjwa akiwa amepumzika baada ya kupatiwa huduma
Miongoni mwa waliopata ajali akiwa kitandani wodini
Dada huyu akiwa ametulia kitandani kumuomba mungu ampe ahueni
Majeruhi wawili katika kitanda kimoja kama inanvyoonekana
No comments:
Post a Comment