02 November 2013

KWAPA LA MPENZI WANGU LINANUKA ....!! KILA NIKIWA NAYE LAZIMA NIPIGE CHAFYA SANA...USHAURI JAMANI NIFANYAJE..??

 


Mimi  ni  mdada  mwenye  umri  wa  miaka  27.Nina  uhusiano  wa  kimapenzi  na  mwanaume  mwenye  umri  wa  miaka  33  kwa  muda  wa  miezi  mitano   sasa.
Tatizo langu  ni  kuwa  kila  tufanyapo  mapenzi  huwa  nashikwa  na  chafya  kali  sana.Chanzo chake  ni  kwapa  ya  mpenzi  wangu ..

Nashindwa  kuelewa  tatizo  ni  nini  maana  kwenye  suala  la  usafi  sijaona  kama  ni  tatizo  kwake.Kabla  ya  tendo  huwa  tunaoga  pamoja  na  humsugua  sana  tu..

Tukishafika  kitandani  kwapa  hutoa  harufu  utadhani  hajaoga  mwezi  mzima, yaani  hata  hamu  ya  tendo  huniishia, kuziba  pua  nashindwa, nikihofia  kwamba  atanielewa  vibaya.Kwa  hiyo  huwa  navumilia  tu  ili  mradi  amalize  hamu  yake...

Jamani, naombeni  msaada  ili  uhusiano  wangu  usivunjike  maana  bado  nampenda  mpenzi  wangu.

Maadam A. 

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname