13 November 2013

JE UNAJUA KUWA DIAMOND ALILIPWA SH. 10,000 KWENYE SHOW YA FIESTA?? SOMA HAPA..!!





Msanii maarufu kwenye tasnia ya muziki kwa sasa DIAMOND alilipwa tsh 10,000/- tuu katika FIESTA 2009 ambapo alifanya show Kali iliokubalika na wadau wa muziki Tanzania. Hayo amebainisha mwenyewe wakati akihojiwa na gazeti Mwanaspoti Tanzania tarehe 7-Nov-2013, ambapo malipo kamili ilikuwa tsh 50,000/- tuu,
yeye pamoja na wacheza show wake wanne ambapo kama utagawanya sawa kwa kila mmoja utapata kiasi cha shilingi kumi elfu tuu 10,000/-.
Show hiyo iliokuwa na msanii toka America buster ryhims ambayo ilijaza watu sana Mimi mwenyewe nikiwemo.. ilihusisha wasanii wengine wa Tanzania, waliokuwapo ni pro Jay, malow, Cpwaa, B band nawengineo.
My take.. kumbe ndo maana bifu aziishi na wazee wa maghorofani kama uhuni wenyewe uko hivi nahisi kizunguzungu, Nb, mkiona msanii anaomba msaada mpeni bila kinyongo wala maswali,vinginevyo wote tuwanafikii tuu..

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname