Ndugu
waandishi wa habari, Jukwaa limewaalika hapa katika muendelezo wake wa
kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
mh. -Dr. John Magufuli. Hivi karibuni mh. Rais ameongoza mapambano
makubwa ya kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi na kuwachukulia hatua wale
wote ambao wamehusika kuliingizia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi
yaliyopotea. Tunaunga mkono juhudi hizi za Rais wetu na tunamuhakikishia
kuwa Jukwaa linamuunga mkono na kwamba tunaomba azidishe kasi zaidi ili
wale wote waliokwepa kodi wakamatwe, walipe na kufikishwa katika vyombo
vya sheria bila huruma yoyote.
No comments:
Post a Comment