KIFO
cha Mchungaji Christopher Mtikila (65) aliyezaliwa mwaka 1950, kimezua
utata ambapo baadhi ya watu wa karibu na mwanasiasa huyo wanadai kwamba
‘ameuawa’.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini,
mmoja wa watu hao amesema licha ya Jeshi la Polisi nchini kusema kwamba
kifo hicho kilichotokana na ajali iliyosababishwa na mwendo kasi, lakini
kuna kila dalili za ‘mkono wa mtu’ kutokana na harakati za mwanasiasa
huyo katika masuala ya kijamii, kitaifa na kimataifa.
No comments:
Post a Comment