27 June 2015

KINACHOMPONZA DIAMOND PLATINUMZ NI UTANZANIA WAKE! SOMA KWA KINA HAPA..


Diamond Platnumz. MOJA ya tatizo kubwa la kitaifa ambalo Watanzania tunalo ni kukosa uzalendo, sumu hiyo ilianza kututafuna taratibu na sasa inazidi kukua katika maeneo mengi. 
Ukitaka kuamini tazama jinsi wacheza soka wanavyocheza wakiwa timu za taifa, angalia baadhi ya viongozi wa siasa na serikalini wanavyofanya ufisadi kwenye mali za uma bila hata aibu. 
Msanii wa Kitanzania, Diamond Platnumz ni mmoja wa wanaowania Tuzo za MTV Mama 2015, inaeleweka wazi kuwa hakuna anayelazimishwa kumshabikia msanii fulani lakini kumekuwa na idadi kubwa ya Watanzania wanaojitokeza na kumpinga Diamond kimataifa huku wakimuunga mkono Davido wa Nigeria. 
Licha ya Diamond kufanya kazi na wasanii wa Nigeria lakini hakuna mashabiki wa Nigeria wanaojitokeza na kutangaza kimataifa kumuunga mkono Diamond katika tuzo hizo, hiyo inaonyesha jinsi ambavyo uzalendo wa Watanzania unavyoelekea shimoni.  

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname