Diamond
Platnumz. MOJA ya tatizo kubwa la kitaifa ambalo Watanzania tunalo ni
kukosa uzalendo, sumu hiyo ilianza kututafuna taratibu na sasa inazidi
kukua katika maeneo mengi.
Ukitaka kuamini tazama jinsi wacheza soka
wanavyocheza wakiwa timu za taifa, angalia baadhi ya viongozi wa siasa
na serikalini wanavyofanya ufisadi kwenye mali za uma bila hata aibu.
Msanii
wa Kitanzania, Diamond Platnumz ni mmoja wa wanaowania Tuzo za MTV Mama
2015, inaeleweka wazi kuwa hakuna anayelazimishwa kumshabikia msanii
fulani lakini kumekuwa na idadi kubwa ya Watanzania wanaojitokeza na
kumpinga Diamond kimataifa huku wakimuunga mkono Davido wa Nigeria.
Licha
ya Diamond kufanya kazi na wasanii wa Nigeria lakini hakuna mashabiki
wa Nigeria wanaojitokeza na kutangaza kimataifa kumuunga mkono Diamond
katika tuzo hizo, hiyo inaonyesha jinsi ambavyo uzalendo wa Watanzania
unavyoelekea shimoni.
No comments:
Post a Comment