20 April 2015

KWA HILI DIAMOND UMECHEMKA.

Miaka kadhaa nyuma aliibuka msanii mchanga na nyimbo kali na zilizogusa mioyo ya wengi, hisia kali, mashairi yenye mpangilio na hata vina vilivyosimama kwa unadhifu, walilia wenye kulia kwa tungo hizo, wakafurahi wenye kufurahishwa na utunzi huo, vijana wakasema dah!, mshikaji ni noumaa!, ndio, hayo ndo maneno yetu vijana tukimkubali mtu, ila wazee nao wakasema Mungu amzidishie na kumbariki kijana huyu. Ndio, maneno ya wakubwa dawa bwana, na Mungu kweli akatenda, kijana akabarikiwa.
Kwa mara ya kwanza nlimskia na wimbo wake ‘nenda kamwambie’, hatukukaa sawa akaruka hewani tena na wimbo mzuri wa ‘Mbagala’, baada ya hapo akafululiza na vibao kadhaa matata, ikiwemo ‘Nitarejea’, ‘Moyo wangu’ na ‘mawazo’, vyote vi kanigusa, si mimi peke yangu, ila wengi wetu tuliguswa na tungo zake, ndio maana nikasema alipata baraka za vijana na wazee.
Akalivuka lile daraja reefu la hofu linaloogopwa na wengi, ‘kufeli’, na sasa akawa ni mmoja wa waliomaarufu nchini, waliombeza wakamkubali, waliompuuza wakamuona anafaa, hakuwa na baiskeli sasa akamiliki magari ya kifahari, na mengine akayatoa zawadi kwa walioichezea bahati, bado wazee wakambariki.
BOFYA KUSOMA ZAIDI>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname