09 March 2015

Picha: Simba ilivyoichakaza Yanga uwanja wa Taifa



Emmanuel Okwi wa Simba (kulia) akikwatuliwa na beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' katika mechi baina ya timu hizo leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba ilishinda kwa bao 1-0 lililofungwa na Okwi. 

Abdi Banda wa Simba (kulia) akiondoka na mpira huku akikabwa na kiungo Haruna Niyonzima wa Yanga. 

Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' akizozana jambo na mwamuzi wa mechi ya Yanga na Simba, Martine Saanya. 

Kipa wa Yanga, Ally Mustapha 'Barthez' akiudaka mpira huku akishuhudiwa na kiungo wa Simba, Ramadhani Singano (katikati) na beki wa Yanga, Oscar Joshua. 

Beki wa Yanga, Mbuyu Twite akiondoa mpira huku akizongwa na Emmanuel Okwi wa Simba. 

Mashabiki wa Yanga wakionekana kusisitiza jambo katika mchezo huo wa leo kati ya timu yao dhidi ya Simba.

-GPL

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname