15 March 2015

Picha iliyobamba: Enzi Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akiuza Mitumba



Mpendwa msomaji ni matumaini yetu unaendelea kuperuzi mtandao wako wa kijamii wa Kengete blog, siku zote tupo kwa ajili ya kukuletea habari na matukio mbalimbali kwa njia tofauti ambayo yatakuelimisha, kukuburudisha na kukujenga.

Leo katika picha ya siku ama iliyobamba, ni ya Mbunge wa Iringa, mjini, Mh.Mchungaji Peter Msigwa.

 Kwa mujibu wa chanzo cha picha hiyo iliyowekwa na Msigwa mwenyewe, k upitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Facebook na kuipa maelezo haya “Enzi hizo nauza mitumba (mantigo) Iringa MJINI kabla jengo la Tanesco halijajengwa……enzi hizo tuliita kumechisha.”

Mtandao huu umeona si vibaya tukishare historia hii ambayo inaweza kuwapa ujasiri vijana na kutokata tamaa katika kutafuta mafanikio ya ndoto zao.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname