13 March 2015

MKAZI WA KOROGWE, TANGA AIBUKA MSHINDI WA MTOKO WA MBUGANI KWENYE FAINALI YA KAMPENI “TUTOKE NA SERENGETI”















SERENGETI BREWERIES LTD
TAARIFA KWA UMMA
MKAZI WA KOROGWE, TANGA AIBUKA MSHINDI WA MTOKO WA MBUGANI KWENYE FAINALI YA KAMPENI “TUTOKE NA SERENGETI”
12/03/2015, Dar es Salaam, Droo ya mwisho ya kampeni ya Tutoke na Serengeti imemshuhudia mkazi wa Korogwe Tanga Bw. Robert Gabriel Moriale akitangazwa mshindi katika fainali ya kampeni “Tutoke na Serengeti”. Fainali hiyo imefanyika katika ukumbi wa Baa ya Hongera iliyopo maeneo ya Kijitonyama-Dar es salaam karibu na chuo cha Ustawi wa jamii.

 Mshindi huyo alijipatia fursa ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambapo ataongozana na mtu wake yeyote wa karibu kwa muda wa siku tatu huku SBL kupitia bia yake ya Serengeti Premium ndio itahusika kugharamia usafiri, chakula, malazi sambamba na fedha taslim za mshindi kujikimu pindi atakapokua safarini.

Akiongea kupitia njia ya simu mara baada ya kutangazwa mshindi wa mtoko wa mbugani, Bw.Robert  (49)alipokea taarifa hizo kwa furaha na alisikika akishangilia kwa kelele baada ya kuambiwa kwamba amejishindia “Mtoko wa Mbugani”.

Alipoulizwa kama alishawahi kushinda chochote kabla ya zawadi hiyo, Robert alijibu “Nimekuwa nikishiriki tangu mwanzo na nimepata bia za bure nyingi tu pamoja na pungozo la Tsh 300. Lakini hii ya leo kwa kweli sikuitarajia kabisa”
Akiongea wakati wa kufunga kampeni hiyo, Meneja chapa wa bia ya Serengeti Premium Lager , Bwana Rugambo Rodney alisema, “Tumefurahishwa sana na ushindi wa bwana Robert na tunapenda kumshukuru kwa kushiriki na tunaamini aliifurahia bia ya Serengeti Premium ambayo imemletea furaha ya kipekee siku ya leo.

Rodney pia alitumia fursa hiyo kuwashukuru washiriki wote kwa kutumia muda wao wa thamani katika promosheni hii  na kuwapa moyo wale ambao hawakubahatika kushinda mtoko wa mbugani, Bajaj au bia za bure kutokata tamaa na kushiriki tena nyakati zijazo kwani SBL imekuwa mstari wa mbele katika kurudisha kiasi cha faida waliyopata kwa wateja wake. Aliongeza kuwa wateja wakae mkao wa kula kwani kuna kitu kikubwa kinaandaliwa kwa ajili yao.

Wakati kampeni hii iliyodumu takribani miezi minne inafikia tamati, SBL imetoa shukrani za pekee kwa wateja wake wa Serengeti Premium Lager baada ya kushuhudia  washiriki zaidi ya milioni moja wakijaribu bahati zao na kuifanya promosheni ya “Tutoke na Serengeti” kuwa yenye mafanikio  kutokana na muitikio mkubwa na uelewa kutoka kwa wananchi.

Kampeni imewazawadia wateja mbalimbali fursa ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Serengeti wakati wengine wakiondoka na zawadi murua kama vile Limo Bajaj ambazo kwa kiasi kikubwa zitabadilisha maisha yao. Kulikuwa pia na fedha taslim za kila wiki, bia za bure, na punguzo la Tshs300 katika kila bia ya Serengeti Premium.

Promosheni hii ya nchi nzima pia ilipata ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa B-Pesa, wataalamu wa teknolojia mpya ya usambazaji fedha waliochangia Limo Bajaj sita kwa washindi mbalimbali. Pia walihusika na usambazaji wa fedha kwa washindi nchi nzima katika kipindi chote cha miezi mine ya kampeni.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname