DEREVA
wa lori lililokuwa limebeba saruji kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea
Mwanza leo amefariki dunia baada ya lori hilo kupinduka eneo la Sekenke
mkoani Singida. Watu wengine wanne waliokuwa kwenye lori hilo
wamejeruhiwa.
Mmoja
wa mashuhuda wa ajai hiyo ameiambia tovuti hii kuwa chanzo cha ajali
hiyo ni kufeli breki kwa lori hilo lililokuwa likishuka Milima ya
Sekenke na mpaka anaondoka eneo la ajali hiyo bado dereva (marehemu) na
mmoja wa watu waliokuwemo aliyekuwa hai walikuwa bado wamenasa kwenye
lori hilo
No comments:
Post a Comment