18 July 2014

MAZITO YAIBUKA..!! FLORA MBASHA NA MUMEWE HAWAJAPATANA..


Imebainika  kwamba  waimbaji  wa  muziki  wa  Injili  nchini, Flora Mbasha  na  mumewe, Emmanuel  Mbasha  hawajapatana  kama ilivyodaiwa  awali  na  taarifa  zinasema  kuwa  mwanadada  huyo  ameanza  maisha  yake  kivyake  kwa  kupanga  nyumba  nyingine  mbali  na  mumewe.
Habari  za  kuaminika  toka  ndani  ya  familia  ya  Flora  zinasema  kuwa  msanii  huyo  amekuwa  na  wakati mgumu  wa  kumsamehe  mumewe  kutokana  na  tabia  zake  chafu  ambazo  zimekuwa  zikiutesa  moyo  wake  na  sasa  anang'ang'ania  kumchukua  mwanaye.
"Hivi  karibuni  iliripotiwa  kuwa  wanandoa  hao  wamepatana  lakini  ukweli  ni  kwamba  hakuna  kitu  kama hicho,mwanamke  amepanga  chumba  chake  hapa  Dar  es  Salaam  na  kumwachia  kila  kitu  mumewe  ambaye  sasa  ana haha  kumchukua  mwanaye  ili  aishi  naye," kilisema  chanzo  cha  habari.

Lakini  upande  wa  pili, mume  wa  msanii  huyo  hivi  karibuni  alieleza  kuwa  ugomvi  baina  yao  ulianza  kutokana  na  kuchepuka  kwa  mkewe, huku  akipeleka  shutuma  kwa  mchungaji  wa  kanisa  la  ufufuo  na  Uzima, Josephat  Gwajima  ambaye  ni  maarufu  kwa  vitu  ambavyo  ni  tofauti  na  huduma  zake.Soma zaidi>>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname