28 April 2014

PICHA MTOTO ALIYEAJIRIWA ADAI KUTESWA

Mtoto mwenye umri wa miaka (14) ambaye ni mwenyeji wa Rombo mkoani Kilimanjaro anayeripoti manyanyaso kutoka kwa mtu anayedaiwa kuwa bosi wake. 

Mtoto mwenye umri wa miaka (14) anadaiwa kuajiriwa akiwa na umri mdogo kinyume cha sheria za kazi kisha kupokea kipigo na manyanyaso kutoka kwa mtu anayedai ni bosi wake aliyemtaja kwa jina moja la Agness.

Kwa mujibu wa mashuhuda, mbali na kuwepo kwa malalamiko ya unynyasaji juu ya mtoto huyo, siku ya tukio mwajiri wake alimpa kipigo kwa madai kwamba alimuibia shilingi laki saba dukani alikomwajiri maeneo ya Mwananyamala, Dar hivi karibuni.
 Mtoto huyo ambaye ni mwenyeji wa Rombo mkoani Kilimanjaro alizama jijini Dar na kuajiriwa katika duka hilo mwanzoni mwa mwezi Novemba, mwajka jana.
 Akizungumza na mwanahabari wetu kwa masikitiko, mtoto huyo alisema tangu aajiriwe na mama huyo hajawahi kulala nyumbani bali alikuwa akilala hukohuko kwenye duka ambalo ni dogo halafu limejaa vitu vingi na alikuwa akifungua saa 12:00 asubuhi na kufunga saa 5:00 usiku kila siku.
Bosi wa mtuhumiwa, aliyefahamika kwa jina moja la Agness.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname