06 December 2013

HUYU POLISI AAMUA KUJIUA BAADA YA KUKOSEA KUTUMA SMS.ALITAKA AMTUMIE MPZ WAKE BAHATI MBAYA IKAENDA KWA MUME WAKE

Mwanamke Polisi aliejiua baada ya kukosea msg ya mpenzi wake na kutuma kwa mume wake Dec 5 2013Mwanamke huyu aitwae Gail Crocker ambae alikua Polisi nchini Uingereza imefahamika kwamba alijiua baada ya kumtumia mume wake meseji badala ya kumtumia mpenzi wake ambae alikua polisi mwenzake.

Kwenye msg yenyewe, Gail aliandika kumshukuru mpenzi wake kwamba aliinjoy walipotoka pamoja usiku mmoja, na kumwambia ‘natamani tungekua tunafanya hivi mara kwa mara’
Taarifa imesema Askari huyu ambae ni mama wa watoto wawili alikua akishiriki kwenye penzi la nje na askari mwenzake wakati mumewe akiwa kwenye safari za kibiashara ambapo baada ya kukosea msg aliamua kujiua kwa kunywa vidonge vingi na kujilaza kwenye buti ya gari.

Hata hivyo pamoja na Mwanamke huyo kutoka nje ya ndoa, mume wake ambae wamekua kwenye ndoa kwa miaka 30, Peter Crocker mwenye miaka 49, amesema Gail alikua Mwanamke wake wa maisha.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname