LIGI KUU ENGALND : MAN UTD USO KWA USO NA ARSENAL
leo
ndo leo kuna mechi kati ya Arsenal na Machester United je ni nani
ataibuka na ushindi?basi fatilia hapa hapa matukio yatakayokuwa
yakiendelea katika mchezo huo utakao pigwa majira ya saa 19:10 kwa saa
za Tanzania kuelekea mechi hii Arsenal ni Vinara wa Ligi na wana Pointi
25 kwa Mechi zao 10 za Ligi wakiwa Pointi 5 mbele kileleni na hawajafungwa katika Mechi zao 14 kati ya 15 za Ugenini.
Ushindi
wao wa mwisho umekuja Jumatano huko Germany walipoifunga Borussia
Dortmund Bao 1-0 kwenye Mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Wenger anaamini
Mechi yao hii ya Old Trafford ni moja ya Mechi zao ngumu.
Wenger
amesema: “Hii ni moja michezo ambazo zinakufanya ujenge imani na kupata
mafanikio ukishinda. Hivi karibuni hatujafanya vizuri Uwanja ule. Kitu
muhimu ni kuamini uchezaji wetu na umahiri wetu. Ni nafasi nzuri
kuonyesha sasa tuna mafanikio.”
No comments:
Post a Comment