09 November 2013

HII VIDEO MPYA YA BABY MADAHA YAZUA UTATA KUTOKANA NA KUWA NA VITENDO VYA KI FREEMASON NDANI YAKE

Video ya muziki ya mwanadada Muigizazji na mwanamuziki Baby Madaha “Squeeze me tight” imeanza kuzua utata kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutazamwa na watu wengi sana kwa muda mfupi tangu ilipowekwa hewani kwenye mtandao wa youtube.
Video hiyo ambayo imerekodiwa huko nchini Kenya chini ya Studio za Candy n’ Candy Records ina mahadhi ya kijamaika flani hivi  na pia ukiichunguza kwa umakini zaidi ina vionjo flani vya “kizombie” na pia ipo “too sexy” kitu kilichotafsiriwa kama mambo yale  ile “dini ya wavaa suti” na sababu ya video hii kutazamwa sana. Tuliamua kumtafuta baby Madaha mwenyewe ili ajibu tuhuma hizi lakini kwa bahati mbaya simu yake ya mkononi likuwa inatumika muda wote tuliompigia. Tutaendelea kumtafuta na kuwajulisha atakayosema.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname