WOLPER ANASWA AKITWANGA MBEGE
MWANADADA
anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper
Massawe ‘Gambe’ ameamua kudumisha mila na desturi baada ya kupiga picha
akiwa anakunywa pombe ya kienyeji aina ya mbege.Wolper alitundika
picha hiyo katika mtandao wa Kijamii wa Instagram akiwa ameshikilia
kikombe maarufu kinachotumiwa na watu wa Kilimanjaro kwa ajili ya
kunywea pombe aina hiyo na kuambatanisha na maneno kuwa anadumisha mila.
“Nyumbani Arusha nikinywa wine nitakosea jamani, leo mbege tu Wachaga mtanielewa tu,”aliandika Wolper.
Baada
ya kuweka picha na maneno hayo watu mbalimbali walionekana kumfagilia
staa huyo na kumsifu kwamba ameonesha kujali mila tofauti na watu
wengine pindi wanapokuwa mastaa huzibeza mila zao.
Mashabiki wengi walikuwa wakimpongeza kwa kumuandikia maneno kwa lugha ya Kichaga kuonesha kwamba wamemkubali