Tukio hilo la kushangaza na la aina
yake, lilitokea Agosti 29, mwaka huu, majira ya saa 12:00 asubuhi baada
ya kugunduliwa na mfanyabiashara Ester Musa (28) likiwa limetelekezwa
kwenye mlango wa mgahawa wake.
Jeneza hilo linaaminika kufukuliwa na watu wasiofahamika kwenye moja ya makaburi eneo la Mahina jijini hapa.
Akizungumza kuhusiana na tukio hilo,
Ester anayemiliki na kuendesha mgahawa alisema, alifika katika eneo lake
hilo la biashara, ghafla akapigwa na mshangao baada ya kuona jeneza
likiwa mbele ya mlango wa mgahawa wake.
“Nashindwa kujua nini maana ya tukio
hili sababu hivi karibuni nilikuta barua imebandikwa ukutani ikinitaka
nihame kutoka eneo hili, vinginevyo nitaona nitakachofanyiwa. Leo
nimekuta jeneza mlangoni,” alisema Ester na kuongeza;
“Tukio hili nalihusisha na imani za
kishirikina lakini kubwa linachangiwa na wivu wa kibiashara.Tangu
lizaliwe sijawahi kuona jambo kama hili. Hapa sijawahi kugombana na mtu
yeyote nashangaa kufanyiwa kitendo cha namna hii katika eneo la biashara
yangu.”
Mwenyekiti wa mtaa huo, Anthony Deus
alisema kitendo cha kufukua mwili wa marehemu tena mtoto mchanga, si cha
kibinadamu na ni tukio la kusikitisha katika jamii, hivyo
watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
Kaimu Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mwanza,
ACP Christopher Fuime, alikiri kuwapo kwa tukio hilo na kusema hakuna
mtu aliyekamatwa akihusishwa nalo.
“Tunaendelea na uchunguzi lakini hadi
sasa hakuna aliyekamatwa akihusishwa na tukio hili la kusikitisha…
wananchi wameuzika upya mwili wa mtoto huyo,” alisema
No comments:
Post a Comment