12 February 2016

TAMBUA JINSI YA KUTOA SUMU MWILINI

Sumu ni kitu chochote kile ambacho katika mwili huhatarisha utendaji kazi wa mifumo au viungo vya mwili na huweza kupelekea kifo.

Kwa kutegemeana na namna ambavyo sumu huuathiri mwili, tunapata makundi mawili ya sumu; Kundi la kwanza ni aina za sumu ambazo husababisha madhara yasiyorekebishika au tuite ulemavu wa maisha (Irreversible effects), na kundi la pili ni aina za sumu zinazosababisha madhara yanayoweza kurekebishika (Reversible effects).

Miongoni mwa madhara yasiyorekebishika yanayoweza kusababishwa na kundi la kwanza la sumu ni pamoja na, makovu katika ngozi, upofu, matatizo ya akili, matatizo ya damu, kulemaa au kupooza viungo na kuwa kiziwi.

Kundi la pili la sumu husababisha madhara yanayoweza kurekebishika au kutatulika baada ya muda fulani, mfano uvimbe, kuwasha kwa ngozi, ngozi kuwa kavu sana, kutokwa na majibu pamoja na sehemu za mwili kubadilika rangi.

Mpenzi msomaji, kuna vyanzo viwili vya sumu mwilini; chanzo cha kwanza ni kupitia vitu ambavyo vipo nje ya mwili, binadamu huvitumia na matokeo yake humuathiri. Vitu hivi MTU huvitumia pengine kwa kujua au kutokujua kuwa kwake ni sumu, mfano matumizi ya kemikali aina ya zebaki ( mercury) katika shughuli za migodini, uangalifu au umakini mkubwa wahitajika pindi utumiapo kemikali hii kwani huweza kukupa madhara katika mapafu na moyo. Sumu nyingine hujitokeza kwa kukosa au kutozingatia maelekezo tunayopewa juu ya utumiaji salama Wa Dawa za kutibu magonjwa, mtu anazidisha dozi, au ni mama mjamzito lakini anatumia Dawa ambayo siyo salama kwa kiumbe kilichopo tumboni, matokeo yake ni kuhatarisha maisha ya mjamzito, mtoto tumboni au kuja kujifungua mtoto mwenye ulemavu usio rekebishika.

Chanzo cha pili cha sumu ni miili yetu wenyewe, ni katika hali ya kawaida mwili unazalisha sumu mbalimbali kupitia mifumo yake ya Kazi, mfano katika uvunjwaji na usambazaji Wa chakula mwilini, mifumo ya hewa, utengenezaji wa damu, katika Kazi zote hizi na nyingine ambazo mwili hufanya, kuna baadhi ya sumu huzalishwa pamoja na kemikali (free radicals) nyingi ambazo hazitakiwi ziendelee kukaa mwilini, kwani huathiri utendaji Kazi wa kawaida wa mwili.

Uondoaji wa sumu mwilini hutegemeana na aina ya sumu yenyewe. Njia ya kwanza ni matumizi ya Dawa za kuivunja nguvu ile sumu husika ambapo kitaalamu hujulikana kwa jina la antidote, hapa ni baada ya uchunguzi kufanyika na kugundua aina ya sumu iliyokuathiri na kisha utapewa dawa kulingana na majibu ya uchunguzi wa kitaalamu.

Njia ya pili inayoweza kutusaidia kuondoa sumu na hasa zile zinazozalishwa mwilini ni matumizi ya vyakula bora, hivi ni vyakula ambavyo kwa asili yake huwa na virutubisho ambavyo huvunja vunja na kuondoa sumu mwilini, vyakula hivi kitaalamu huwa na vitu vinavyoitwa antioxidants, ambavyo huulinda mwili dhidi ya kemikali hatarishi zinazozalishwa mwilini. Virutubisho hivi ni pamoja na Vitamin A, Vitamini C na Vitamini E. Vitamini hizi hupatikana katika mboga za majani na matunda, mfano mchicha, spinachi, karoti, matembele, machungwa, nanasi, maembe, machenza pamoja na mafuta ya mimea mfano alizeti.

Ili miili yetu iweze kufanya kazi vizuri na tuendelee kuwa na afya njema, inabidi tuepukane na sumu hizi, pale inapo tulazimu zitumike (mfano zebaki, migodini), basi tuzidishe umakini katika kujilinda afya zetu, na pia tubadilishe aina ya maisha au ulaji wa vyakula, matunda na mboga za majani ni walinzi wakubwa sana wa afya zet

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname