10 February 2016

Salam Jabir Nae Aibuka Kwenye Malumbano ya Video Mpya ya Ali Kiba Baada ya Baadhi Kuiponda...Asema Haya

Mtangazaji wa kipindi cha Mkasi ambacho kinarushwa kupitia ting'a namba moja kwa vijana (EATV) Salama Jabir amefunguka na kuwataka watanzania kuthamini na kuheshimu watu ambao wanajituma kufanya mambo katika kazi zao.

Salama amesema kuwa kazi ya msanii siku zote ni sanaa ambayo unaweza kuipenda au kutoipenda.
Salama Jabir amesema hayo kupitia Account yake ya Twitter kufuatia baadhi ya maoni ya mashabiki ambao wamekuwa wakiwaponda wasanii wa bongo pindi wanapokuwa wanatoa kazi zao hususani video huku mashabiki wengine wakienda mbali na kuponda au kuzungumzia jambo kama wao wana maarifa ya jambo hilo.

"Kazi ya msanii ni Sanaa... Usingiingilie!! ni aidha utaipenda au hutaipenda simple!! Kama rahisi fanya na wewe tuone Respect kwa wanaojituma" Amesema Salama

Imekuwa ni kawaida kwa mashabiki kuponda kazi za wasanii na kuwatusi kupitia mitandao yao ya kijamii jambo ambalo linakuwa linakatisha tamaa baadhi ya wasanii na kuwaumiza kwani maneno ambayo mashabiki huwa wanatumia ni makali na ya kukatisha tamaa.

Hali hii mara nyingi imekuwa ikisababishwa na makundi ya mashabiki maarufu kama Team, kuna watu wanaweza kuponda jambo ili mradi tu kwa sababu yeye si shabiki wa msanii fulani na wapo wengine wanafanya hivyo kwa lengo ya kukomesha, huku wengine wakitaka wasanii waendelee kuleta video za aina fulani pekee na ukifanya vinginevyo wanaona umekosea kwa sababu ndicho kitu walichozoea kifupi hawataki kukutana na kitu cha iana mpya.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname