Mbunge
wa CCM kupitia kadi ya Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Arusha,
Catherine Valentine Magige . IMEFICHUKA! Madai ya Mbunge wa Viti Maalum
(CCM) Mkoa wa Geita, Vicky Paschal Kamata kuwatumia meseji za kashfa
wabunge wenzake, Lucy Thomas Mayenga (CCM) na Catherine Valentine Magige
(UVCCM)Mkoa wa Arusha sasa mambo hadharani.Kwa mujibu wa chanzo chetu,
wabunge hao warembo wako katika vita baridi ikiendeshwa chini kwa chini
kwa Cathy (pichani) na Lucy kudai kwamba wamekuwa wakitumiwa meseji
zenye kejeli na kashfa nzito kutoka kwa mheshimiwa Vicky.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, licha ya sababu kutokuwa wazi sana,
lakini madai ni kwamba wana bifu linalokimbilia mwezi wa nne sasa.
“Unajua si rahisi wao kuweka wazi bifu lao, lakini wenyewe watakuwa
wanajua nini kiini, ukifuatilia utagundua kuwa maisha yao yamekuwa ni ya
vikundivikundi, akina Lucy wana kundi lao na Vicky ana la kwake,”
kilisema chanzo hicho.
Mbunge wa CCM kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana, Lucy Thomas Mayenga
No comments:
Post a Comment