Hivi wanawake ni watu wa aina gani?
naombeni ushauri jamani, nilikuwa na mpenzi akanisaliti akaenda kuolewa
na lijibaba nikatafuta mwingine,nimezaa nae mtoto mmoja natunaishi kwa
furaha.cha ajabu ameanza kunitumia mesege,mojawapo imeandikwa hivi
nanukuu "Najua nilikukosea samahani sana ila
naomba umuache huyo mwanamke, amin
nitamlea mtoto wako kama wakwangu
kumbuka unafahamika mbaka nyumbani familia yangu inanicheka kwa
nilichokifanya".huyu mwanamke ninaeshi nae kaona hiyo massage kaniambia nimsamehee na yuko radhi kuondoka....Sasa nifanyaje nishaurini
By Silvester Limota

No comments:
Post a Comment