30 October 2013

HIZI NDO FUJO ZILIZO FANYWA NA MASHABIKI WA MBEYA CITY KATIKA MCHEZO DHIDI YA PRISON


1
Taarifa kutoka 87.8 Mbeya zinaamplfy kwamba mashabiki wa Mbeya City wamelishambulia gari la wachezaji wa Prisons na kumuumiza mchezaji mmoja ambapo pia walivunja vioo vya  gari aina Toyota Coaster na magari mengine yaliyokuwa kwenye msafara wa timu hiyo ikitoka uwanjani baada ya kufungwa na Mbeya City kwa mabao 2-0.

mbeyayetu.blogspot.com wameripoti kwamba Mashabiki hao walilishambulia magari hayo na kuyavunja vioo na baada ya hapo wakakimbilia kusikojulikana.

Mmoja wa maofisa wa Prisons alisema ana uhakika kuwa waliofanya hivyo ni mashabiki wa Mbeya City kwa kuwa walikuwa wamevaa jezi za rangi ya zambarau ambayo huvaliwa na timu hiyo.
2
3
4
5
6Hapa chini ni baadhi ya fans Mbeya City wakiwa wamebeba jenela la timu ya Prisons, chini ya hii picha ni baadhi ya picha wakishangilia magoli uwanjani
9
8
7 
credit-mbeyayetublog

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname