MTOTOo wa miaka miwili amefariki baada ya baba yake kudaiwa kumtupa
kitandani - na kusababisha mtoto huyo wa kiume kujibamiza kichwa chake
ukutani - kwa sababu alitapika.
Mama wa Jayden Morales Villegas
alikubaliana na uamuzi wa kumtoa mtoto huyo kwenye mashine kuokoa maisha
Jumapili mchana, siku tano baada ya kudaiwa kupas
uka akiwa mikononi mwa
baba yake, Angel Villegas, mwenye umri wa miaka 29.
Shambulio hilo linadaiwa kutokea wiki mbili tu baada ya Jayden na
kaka zake watatu kutolewa kwenye mikono ya uangalizi wa mama yao na
Idara ya Watoto na Familia na kuhamishiwa kwa baba yao.
Villegas, baba wa watoto tisa, alikuwa akimtunza mtoto huyo na
baadhi ya ndugu zake kwenye makazi yake huko Homstead, Florida Jumanne
ndipo mtoto huyo, ambaye alikuwa akisumbuliwa na baridi, alitapika
wakati wa chakula cha usiku.
Alichanganywa na mtoto wake na kumtupa kitandani, kumsababishia
mtoto huyo kugonga kichwa chake ukutani. polisi walisema. Alimkuta mtoto
huyo akiwa hajitambui siku iliyofuata, kiapo chake kilisema.
Mtoto huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Watoto ya Miami, ambako
alitangazwa ubongo haufanyi kazi na kuwekwa kwenye mashine ya kuokoa
maisha. Lakini alitangazwa kufariki Jumapili Saa 7:30 mchana.
"Inauma mno, alikuwa tu mwanangu," mama wa Jayden, Vanessa Morales
alieleza. "Nilimweleza tu awe jasiri, kwamba tunampenda na kaka zake
wanampenda na kwamba kamwe sitaweza kumsahau."
Villegas alikamatwa na mashitaka yake yameongezwa kutoka kujaribu kuua hadi kuua na kudhalilisha mtoto kwa kiwango cha juu.
Morales aliongeza kwamba alishitushwa na kukamatwa huko.
"Chizi, anayechukiwa na aliyechanganyikiwa kabisa sababu sikufikiria
kabisa angeweza kufanya kitu kama hicho," alisema. "Kwanini hakuelekeza
hasira zake kwingineko mbali na mtoto huyo wa miaka miwili, hususani
mtoto wake, mtoto wake."
Ukurasa wake wa Facebook ulitawaliwa na picha zake na watoto wake, wakiwamo watoto wawili wa kiume na mtoto wa kike.
Watoto wote wa Villegas na wa Morales wamebaki chini ya uangalizi wa Idara hiyo ya Watoto na Familia.
Villegas anashikiliwa kwa dhamana ya Dola za Marekani 110,000 lakini
kama akilipa kiasi hicho, atawekwa chini ya ulinzi nyumbani.
No comments:
Post a Comment