Shirika la Umeme nchini, Tanesco limebaini wizi wa umeme nyumbani kwa
Wema Sepetu. Mafundi wa shirika hilo waliambatana na waandishi wa habari
hadi kwenye nyumba hiyo na kubaini kuwa umeme unaingia moja kwa moja
kwenye nyumba bila kupita kwenye mita. Wakati mafundi hao wameingia
nyumba hiyo walimkuta Idris Sultan ndani aliyejaribu kuwasihi wasiukate
umeme. Kukutwa kwa Idris kwenye nyumba hiyo kumetia mafuta zaidi tetesi
za kuwa wawili hao wana uhusiano.
No comments:
Post a Comment