Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akisalimiana na kumpongeza Nahodha wa Timu ya Taifa Stars, Nadir Haroub
'Canavaro', baada ya mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi Kombe la dunia
kati ya Taifa Stars na Algeria
uliochezwa jana. Katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya 2-2, mabao
ya Stars yalifungwa na Elias Maguli na Mbwana Samatta.
Akizungumza
na wachezaji hao baada ya mchezo huo, Mhe. Samia,aliwataka wachezaji na
viongozi wa Stars kutovunjika moyo kutokana na matokeo ya mchezo huo,
na kuwataka kuongeza juhudi na kujituma zaidi katika mchezo wa marudiano
ili ukweza kupata matokeo mazuri zaidi.
''Japo
mmefungwa lakini tumewaona jinsi mlivyojituma, msivunjike moyo na
matokeo ya mchezo, kwani tumeowana mlivyocheza kwa kujituma, hivyo
naamini hata ugenini mtaweza kupata matokeo mazuri zaidi mkiwa na moyo
huo huo wa utaifa, juhudi na kujituma,
Mtangulizeni
mungu kwa kila jambo na kwa uwezo wake naamini mtaenda kufanya vizuri
katika mchezo wa marudiano, na nawatakieni safari njema leo usiku
kuelekea mchezo huo wa marudiano, sisi wazee wenu na Watanzania wote
tupo nyuma yenu tunawaombe muweze kuwatoa waarabu hawa wenye fitina kali
katika mchezo wa Soka''. alisema Mhe. Samia
No comments:
Post a Comment