BASI tena! Kifo cha ajali ya gari cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (DP) na Kiongozi wa Kanisa la Full Salvation, Mchungaji Christopher Mtikila kimewaacha wananchi na majonzi makubwa lakini nyuma yake, Uwazi limebaini maswali 10 tata kuhusu ajali hiyo.
Ajali hiyo ilitokea saa kumi na mbili asubuhi ya Jumapili iliyopita, eneo la Msolwa, Chalinze wilayani Bagamoyo, Pwani ambapo gari aina ya Toyota Corolla lenye namba za usajili T 189 AGM lilipoteza mwelekeo na kuingia bondeni. Mtikila alipoteza maisha papohapo huku watu watatu, akiwemo dereva wa gari hilo wakinusurika.
No comments:
Post a Comment