MASHALI AMDUNDA BIGRIGHT NA KUMPORA SIMU NA PESA
Bondia
Thomas mashale wa manzese jijini Dar es salaam alifanya kitendo cha
kusikitisha na kushangaza umma katika ukumbi wa friends corner uliopo
Manzese ,pale alipomvamia katibu wa ngumi za kulipwa nchini Ibrahim
Kamwe (bigright) kumpiga na kumpora simu na pesa. Akizungumza na vyanzo
habari hizi Ibrahim kamwe alisema.”Nilikuwepo ukumbini hapo
friends corner nikishuhudia mpambano wa Jonas Segu na idd Pearali kwa
kuwa watu walikuwepo ni wengi mno na pale mbele kulikuwa na fujo za
ushangiliaji nikaona
ni bora nirudi nyuma kabisa ili nishuhudie kwa mbali , ghafla alitokea
bondia huyo Thomas mashali akiwa na wenzake wanne akanishika mikono na
wenzake kuanza kunisachi nilimputa mikono ili nizuie mifuko ndipo
aliponipiga ngumi kali ya kidevuni na kichwani, watu walio karibu
walipotugeukia sisi mashali na wenzake waliondoka haraka na kutokomea na
simu yangu na kipochi akiniacha na maumivu ya kidevu.
No comments:
Post a Comment