Akizungumza
na wananchi katika uwanja wa Ihumilo Nkome jimbo la Geita jioni hii
Magufuli amesema kwamba Chama cha Mapinduzi kinatarajia kupata ushindi
mnono katika uchaguzi mkuu utakaofanyika jumapili ya wiki hii nchini
kote.
Amesema
kwamba kila anakopita wananchi wanazungumza Magufuli, akitolea mfano
Arusha katika majimbo ya Arusha mjini, Monduli na Mbeya sehemu ambayo
inadaiwa kuwa ni ngome ya upinzani pamoja na Visiwani Zanzibar sehemu
ambayo Chama cha Mapinduzi inakumbana na ushindani mkali kutoka chama
cha CUF.
Akizungumzia
jimbo la Geita Magufuli amesema kwamba atahakikisha kuwa jimbo hilo
litakuwa jipya ikiwa wananchi hao watampa ridhaa ya kuchaguliwa kuwa
rais wa Jamhuri ya Muungano katika uchaguzi mkuu ujao ambao utafanyika
jumapili ya wiki hii.Katika mkutano huo Magufuli amewataka wananchi
katika kanda hiyo kuachana na imani potofu ya kuwaua albino kwa kudhani
kwamba wataweza kupata utajiri au kuvua samaki wengi suala ambalo
amedai halina ukweli wowote.
Katika hatua
nyingine Magufulia amemnadi mgombea ubunge ambaye anadaiwa alikuwa ni
moja wa marafiki wa mgombea urais wa Ukawa maarufu kama King Msukuma.
No comments:
Post a Comment